• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Monduli District Council
Monduli District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Malengo
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Eneo la Utawala
      • Tarafa
      • Kata
      • Vijiji
    • Idara
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Idara ya Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwezekaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Onana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelezwa
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria ndogo
    • Mipango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI IDARA YA AFYA MONDULI WAPEWA MAFUNZO

Posted on: September 12th, 2024

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Monduli Dkt. George Kasibante Leo Septemba 12, 2024 amefungua rasmi mafunzo ya siku tatu (3) yaliyo dhaminiwa na TANDIA Internation (NGO) kwa madaktari na wauguzi wa Idara ya Afya Wilayani humo,  yenye dhima ya kuwawezesha watumishi hao kujikinga na magonjwa ya kuambukizwa  yanayotokana na utengevu na utupaji taka za hospitalini ovyo.  

Akifungua mafunzo hayo Dkt. Kasibante amewaeleza watumishi hao kuwa kupitia mafunzo haya mtaweza kukumbushwa namna bora ya kujilinda na maambukizi ya magonjwa ambayo mngeweza kuyapata kutokana na utengevu na utupaji taka mbovu katika mazingira yenu ya kazi, hii ni sambamba na kuwakumbusha suala la usafi mahali mnapofanyia kazi kwani kufanya usafi eneo lako la kazi haikuondolei cheo chako bali kukazia usafi, unadhifu na utoaji wa huduma bora kwa Wananchi.

                                                                                                        

 Aidha, Dkt. Kasibante amewaeleza watumishi hao juu ya suala la umuhimu wa utoaji huduma bora kwa Wateja na namna ya kuwajali wagonjwa wawapo vituoni kwao, " Tumeona kwamba kupitia mafunzo haya tuwakumbushe suala zima la huduma kwa wateja ili tuweze kupungua malalamiko tunayoyapata kutoka kwa Wateja wetu ambao ni wagonjwa, tutengeneze mazingira mazuri kati watoa huduma na wapokea huduma wetu ambao ni wagonjwa. " amesema Dkt. Kasibante

Ameongeza kusema kuwa tunahitaji vituo vyetu vyote viwe na mahitaji muhimu huku akiwaasa watumishi wote kuwa waaminifu Katika utendaji kazi na kwa matumizi ya rasilimali zilizopo na zinazoendelea kutolewa ili zitumike kwa matumizi sahihi yaliyokusudiwa na Serikali.

Akichangia katika ufunguzi wa mafunzo hayo Bi. Amina Bakari ambaye ni  Mratibu huduma za Maabara Wilaya ya Monduli amesema   "Hatutaki Mgonjwa au Mama mjamzito wakose huduma, ikiwa hakuna vifaa husika njoo utoe taarifa ili kila kituo kiwe na vifaa muhimu hasa mashine za kupima wingi wa damu tuweze kuokoa maisha ya Wananchi wetu."  

Naye Dkt. Sanema Peter Mratibu wa UKIMWI Wilaya ya Monduli (DACC) Kwa niaba ya wapokea mafunzo ameeleza kufurahishwa kwake na mafunzo hayo kwani yatakuwa msaada mkubwa  katika utendaji kazi wao kwakuwa lugha nzuri Kwa mgonjwa humpa matumaini ya kupona haraka na pengine kurudi tena mara anapohitaji huduma hiyo.

Dkt. Kasibante amehitimisha kwa kuwasihi watumishi hao kujitahidi Kila mmoja mahali alipo afanye kazi Kwa bidii na weledi, na ushirikiano kwakuwa sote ni Idara moja ya afya na sote tunalenga kutoa huduma bora kwa jamii.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MODFA YALENGA MBALI-MONDULI

    March 20, 2025
  • MHE.FREDRICK LOWASSA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MONDULI

    March 19, 2025
  • MILIONI 240 ZANUFAISHA KIJIJI CHA IRIMORIJO KWA MRADI WA MAJI

    March 18, 2025
  • MAFUNZO YA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WAFANYA BIASHARA WAMILIKI WA VYOMBO VYA MOTO NA MADEREVA

    March 18, 2025
  • Angalia zote

Maktaba ya Video

UFUNDISHAJI WA SOMO LA HISABATI KWA VITENDO KWA DARASA LA NNE SHULE YA MSINGI MAZOEZI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • EDWARD MORINGE SOKOINE
  • TAARIFA YA UPANDAJI MITI
  • Historia ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
  • Mto Wa Mbu - Monduli ilivyonufaika na Tsh. Milion 400

Viunganishi linganifu

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya ajira ya Serikali
  • Ofisi ya Rais utumishi na utawala bora
  • salary slip portal
  • Tanzania Safari Channel

Waliotembelea Kiulimwengu

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Monduli District Council

    Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli

    Namba ya simu: +255 - 27- 2538006

    simu ya mkononi:

    Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz

Mawsilano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Malalamiko
    • ramani ya eneo
    • Huduma zetu

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli