• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Monduli District Council
Monduli District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Malengo
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Eneo la Utawala
      • Tarafa
      • Kata
      • Vijiji
    • Idara
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Idara ya Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwezekaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Onana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelezwa
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria ndogo
    • Mipango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MONDULI DC YAADHIMISHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI

Posted on: September 13th, 2025

Ninawataka Maafisa Elimu Kata, Watendaji wa Kata, Maafisa Tarafa kwa pamoja kuwahamasisha na kuwafahamisha Wananchi wote katika maeneo yenu, ili wajue fursa hizi za Elimu ya Watu Wazima na Elimu nje ya mfumo rasmi; mkibainisha umuhimu na manufaa yake kwa Jamii ili kusaidia jamii kuondokana na dhana potofu iliyojengeka kwa wananchi juu ya elimu hii na kuwafanya wengi wenye uwezo kutojiunga nayo.

Hayo yamesemwa leo Septemba 13, 2025 na Mhe. Gloriana Julius Kimath Mkuu wa Wilaya ya Monduli katika Siku ya Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima na Elimu nje ya mfumo rasmi yaliyofanyika katika viwanja vya Polisi Mjini Monduli.

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo Mhe. Gloriana amewashukuru wadau wote wa elimu ya watu Wazima na Elimu nje ya mfumo rasmi akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli na wadau wote waliochangia kufanikisha maadhimisho hayo.

Akisoma taarifa ya Maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bi. Happiness R. Laizer, Mwl. Magreth Muro ambaye pia ni Kaimu Afisa Elimu Sekondari katika Halmashauri hiyo amesema kuwa; awali Wanakisomo hao walijifunza kusoma, kuandika na kuhesabu tu maarufu kama GUMBARU lakini sasa Wanakisomo hao hujifunza na kuunda vikundi tofauti tofauti vya uzalishaji Mali na wengine hupata fursa za kujiendeleza na Elimu ya juu ambapo kwa Monduli Kuna jumla ya vituo 33 yaani 27 vya MEMKWA na 6 vya MUKEJA. kwa mwaka huu wa 2025 Wilaya ya Monduli jumla ya Wanakisomo 551 wamejiunga na Programu ya  MEMKWA ambayo hujumuisha makundi rika mawili kuanzia umri wa miaka 9 hadi 13 na kundi la miaka 14 hadi 17; huku kupitia MUKEJA inayo husisha miaka 18 na kuendelea  wakijiunga watu 1,050.

Ambapo, Wanakisomo hao hujifunza ujasiriamali, ushonaji, useremala, umeme wa majumbani, upishi, upambaji, uongozaji wa Watalii pamoja na kujifunza stadium za kusoma, kuandika, na kuhesabu kwa wasio na stadi hizo.

Mwl. Magreth Muro licha ya kueleza mafanikio makubwa yaliyofikiwa kutokana na utekelezaji wa programu hizo, ameeleza pia changamoto zinazokabili utoaji wa elimu kwa Wanakisomo hao kuwa ni pamoja na dhana potofu ya Jamii kuhusu Elimu husika, wahitaji wa elimu hiyo kuogopa kuchekwa, kuwepo wa vituo vichache, upungufu wa walimu wa ufundi na vifaa.

Kwa upande wake Bi. Suzan Mollel mmoja wa wanufaika wa elimu hiyo Wilayani Monduli, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kusimamia utoaji wa elimu hii na kuomba Jamii kuwa na mtazamo chanya juu ya elimu hii kwani imesaidia katika kuimarisha uchumi wa wengi kwa Maendeleo ya Jamii na Taifa pia.

Kaulimbiu: " Kuza kisomo katika zama za kidigitali kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu. "

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MONDULI DC YAADHIMISHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI

    September 13, 2025
  • MIMI SI MKUU WA MKOA WA KUKAA OFISINI BALI WA KUWAFIKIA WANANCHI KUSIKILIZA KERO ZAO NA KUZITATUA

    September 10, 2025
  • SIMAMIENI NIDHAMU NA KUDHIBITI UPOTEVU WA VIPINDI

    September 02, 2025
  • DC GLORIANA AFUNGA RASMI MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA LA 43/2025 - MONDULI

    August 27, 2025
  • Angalia zote

Maktaba ya Video

UFUNDISHAJI WA SOMO LA HISABATI KWA VITENDO KWA DARASA LA NNE SHULE YA MSINGI MAZOEZI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • EDWARD MORINGE SOKOINE
  • TAARIFA YA UPANDAJI MITI
  • Historia ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
  • Mto Wa Mbu - Monduli ilivyonufaika na Tsh. Milion 400

Viunganishi linganifu

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya ajira ya Serikali
  • Ofisi ya Rais utumishi na utawala bora
  • salary slip portal
  • Tanzania Safari Channel

Waliotembelea Kiulimwengu

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Monduli District Council

    Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli

    Namba ya simu: +255 - 27- 2538006

    simu ya mkononi:

    Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz

Mawsilano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Malalamiko
    • ramani ya eneo
    • Huduma zetu

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli