• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Monduli District Council
Monduli District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Malengo
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Eneo la Utawala
      • Tarafa
      • Kata
      • Vijiji
    • Idara
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Idara ya Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwezekaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Onana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelezwa
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria ndogo
    • Mipango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SIMAMIENI NIDHAMU NA KUDHIBITI UPOTEVU WA VIPINDI

Posted on: September 2nd, 2025

Hakikisheni mnasimamia upotevu wa vipindi pamoja na nidhamu kwa walimu na  wanafunzi  kwakuwa nidhamu nzuri ni chanzo cha ufaulu, na ikiwa mtazingatia ratiba ya vipindi na kuimarisha  mikakati kuelekea mabadiliko makubwa ya ufaulu mliyojiwekea mtaboresha taaluma na ufaulu utapanda zaidi katika Wilaya ya Monduli.

Hayo yamesemwa leo Septemba 2, 2025 na Bi.  Happiness R. Laizer Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri hiyo; wakati akizungumza na Maafisa Elimu Kata pamoja na Walimu Wakuu wa Shule za Sekondari zilizopo Wilayani Monduli katika kikao kazi chenye dhima ya kuweka  mikakati thabiti ya kuboresha na kuinua zaidi kiwango cha Taaluma katika Shule za Sekondari Wilayani humo.

Akisoma taarifa ya Elimu ngazi ya Sekondari Mwl.Given J. Moye ambaye ni kaimu Afisa Elimu Sekondari amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya  ya Monduli ina jumla ya  shule 27 ambapo 16 ni za Serikali na 11 ni shule zisizo za Serikali.

Ambapo Mwl.Given ameeleza kuwa  ufaulu katika Shule zote ni mzuri huku akibainisha matokeo ya mitihani ya Taifa kwa kidato cha pili na cha nne  yanapanda mwaka hadi mwaka ambapo Mwaka  2023 ufaulu ulikuwa asilimia 97.8 na mwaka 2024 ufaulu umeongezeka na kufikia asilimia 98.85 na kupelekea kupata tuzo za pongezi kwa ufaulu mzuri wa viwango vya KPI kwa kidato cha pili nafasi ya kwanza (1) na kidato cha Nne nafasi ya tano (5) Kitaifa kati ya Halmashauri 184.

Kwa upande wake Kimbele Njake Mkuu wa Shule ya Sekondari Manyara, ameeleza mikakati  inayotumika shuleni hapo kuhakikisha wanaondoa daraja "0" na daraja la "4" ikiwa ni pamoja kuhakikisha wanafunzi wanafanya mitihani kwa wingi ikiwemo mitihani ya marudio inayoshindanishwa ya kidato cha kwanza na pili kwa watahiniwa watarajiwa wa kidato cha pili  pamoja mitihani ya marudio ya kidato cha pili na cha tatu  kwa  watainiwa wa kidato cha nne.

Naye Ndg.Raphael Martin Mkuu wa Shule ya Tumaini  Senior Sekondari (binafsi) ameongeza kuwa  mkakati   wake ni kufanya mitihani kwa wingi hasa kutoka shule  zinazofaulisha zaidi ikiwemo St.Francis ambapo hubadilishana uzoefu wa ufundishaji na ujifunzaji.

Sayuni Alex Tarimo Mwenyekiti TAHOSA amewaasa walimu wakuu wote kusikiliza kero na maoni ya wanafunzi kupitia vikao vya madarasa lakini pia kero za walimu wanazokutana nazo darasani na kusimamia mikakati wanaojiwekea ili kupata matokeo chanya.

Bi.Happness R. Laizer amehitimisha kwakuwataka   walimu kufanya hamasa kubwa kwa walimu wenzao mashuleni ili wote kwa pamoja washiriki kikamiifu katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 202

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIMAMIENI NIDHAMU NA KUDHIBITI UPOTEVU WA VIPINDI

    September 02, 2025
  • DC GLORIANA AFUNGA RASMI MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA LA 43/2025 - MONDULI

    August 27, 2025
  • DC GLORIANA AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA LA 43/2025 - MONDULI

    August 27, 2025
  • DC GLORIANA APOKELEWA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO TARAFA YA KISONGO

    August 15, 2025
  • Angalia zote

Maktaba ya Video

UFUNDISHAJI WA SOMO LA HISABATI KWA VITENDO KWA DARASA LA NNE SHULE YA MSINGI MAZOEZI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • EDWARD MORINGE SOKOINE
  • TAARIFA YA UPANDAJI MITI
  • Historia ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
  • Mto Wa Mbu - Monduli ilivyonufaika na Tsh. Milion 400

Viunganishi linganifu

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya ajira ya Serikali
  • Ofisi ya Rais utumishi na utawala bora
  • salary slip portal
  • Tanzania Safari Channel

Waliotembelea Kiulimwengu

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Monduli District Council

    Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli

    Namba ya simu: +255 - 27- 2538006

    simu ya mkononi:

    Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz

Mawsilano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Malalamiko
    • ramani ya eneo
    • Huduma zetu

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli