Vyombo vya Watoa huduma ya maji ngazi ya jamii wilaya ya monduli Vimetakiwa Kuwa mstari wa mbele kusimamia Miradi ya maji inayotekelezwa na Serikali ili kufanikisha adhma ya kufikisha huduma hiyo kikamilifu kwenye jamii.
Wito huo umetolewa na Afisa tawala wilaya ya monduli Ndugu. Anael Mbise Akimwakilisha mkuu wa Wilaya ya Mhe Joshua Nassari katika kikao cha mkutano Mkuu wa mwaka wa vyombo vya Watoa huduma ya maji kilicho fanyika wilaya hapo.
Amesema Serikali inatoa fedha nyingi kufanikisha miradi hiyo lakini kumekua na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya maji jambo ambalo linarudisha nyuma jitihada za kusambaza huduma ya maji
Katika hatua nyingine amemuelekeza Meneja wa RUWASA wilaya ya monduli kuvisimamia vyombo hivyo vifanye kazi kwa Ueledi na kuvivunja mara moja vyombo vivuli visivyo fanya kazi ambavyo amevitaja kuwa chanzo cha ukwamishaji.
Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa kata ya Monduli Juu Mhe. Thomas Meiyan Ametumia kikao hicho kutoa wito kwa wana monduli kuthamini fedha za serikali zinazotolewa kupitia miradi mbalimbali kwa kuitunza.
Nae Katibu wa chama cha Mapinduzi Wilaya ya Monduli Bi Rukia mbasha kwa niaba ya chama cha mapinduzi Amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiletea monduli miradi mingi ya kimaendeleo ikiwemo miradi ya maji.
Aidha Meneja wa RUWASA Mkoa wa Arusha Mwandisi Emmanuel Makaidi akizungumza katika kikao hicho amesema vyombo vya watoa huduma ya maji ndio uti wa mgongo unaosaidia katika uendelevu wa huduma hivyo, amevitolea wito kufanya kazi kwa uadilifu na kusimamia nafasi zao ipasavyo.
Hata hivyo, Meneja wa Ruwasa wilaya ya monduli Ndugu.Neville Daud Msaki akitaja mkakati wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuendelea kutoa huduma bora zaidi katika wilaya nzima ya Monduli, ambapo amesema adi kufikia mwaka 2025 wanatarajia kufikia asilimia 85 za utoaji huduma.
@obedemmanuel
Monduli District Council
Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli
Namba ya simu: +255 - 27- 2538006
simu ya mkononi:
Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli