Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, Bi. Happiness R. Laizer, amewapongeza Afisa Elimu Msingi na Afisa Michezo Wilaya ya Monduli, kwa kusimamia vyema mashindano ya UMITASHUMTA mwaka 2025, ambapo Monduli imeibuka Mshindi wa jumla katika Mkoa wa Arusha ambaye amejinyakulia vikombe 9 na medali 10 ✅
Bi. Happiness R. Laizer ametoa pongezi hizo kwa juhudi, nidhamu na mshikamano wa timu nzima ya Monduli nakusema " ushindi huo unaonesha namna sekta ya elimu na michezo ilivyojipanga kuendelea kuboresha na kuibua vipaji vipya na kuvitunza kwa Wanafunzi wetu kwa faida ya Sekta hiyo. "
Bi. Happiness amehitimisha kwa kuwasisitiza Maafisa hao kuzidi kuhamasisha Wanafunzi Wilayani humo, kushiriki kikamilifu katika Michezo huku akisisitiza kuendelea kuwekeza zaidi katika Michezo kwa kuwa Michezo ni Afya, Michezo ni ajira.
Monduli District Council
Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli
Namba ya simu: +255 - 27- 2538006
simu ya mkononi:
Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli