• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Monduli District Council
Monduli District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Malengo
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Eneo la Utawala
      • Tarafa
      • Kata
      • Vijiji
    • Idara
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Idara ya Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwezekaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Onana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelezwa
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria ndogo
    • Mipango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC GLORIANA AZINDUA CHANJO YA TATU MOJA- MONDULI

Posted on: July 16th, 2025

Ninatumaini  kazi hii mtaifanya kwa uaminifu na uadilifu mkubwa ili kuhakikisha chanjo hizi zinatolewa kwa wahitaji wote ndani ya Wilaya ya Monduli, nami sitamfumbia macho Mtaalamu yeyote atakayebainika kwenda kinyume na maelekezo ya utoaji chanjo hizi.

Hayo yamesemwa mapema leo Julai 16, 2025 na Mhe. Gloriana  Julius Kimath mara baada ya kuzindua rasmi  zoezi la utoaji wa chanjo ya Tatu moja ikiwa ni mwendelezo wa utoaji wa chanjo hiyo iliyozinduliwa rasmi kwa mara ya kwanza na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan huko Mkoani Simiyu.

Akisoma taarifa ya zoezi la utoaji wa chanjo ya Kitaifa kwa mifugo Bi. Pamela Ijumba Mkuu wa Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi amesema kuwa; Halmashauri ya Wilaya ya Monduli imepokea dozi 200,000 za chanjo ya Tatu moja (mdondo, ndui na mafua) kwa kuku,  dozi 225,000 za chanjo ya homa ya mapafu kwa ngombe, hereni 20, 000 kwa ajili ya utambuzi wa ng'ombe, pamoja na hereni 20,000 kwa ajili ya utambuzi wa mbuzi na kindoo.

Aidha, Bi. Pamela amekiri kupokea vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha zoezi hilo ikiwemo jozi 15 za gumboot, overall 15, automatic syringes 25, madeli ( cool boxes) 25, sindano 169 kwa ajili ya ng'ombe, sindano 139 kwa ajili ya mbuzi na kindoo na gloves boksi Moja (1) huku akieleza kuwa utaratibu wa utoaji wa chanjo hizi ni bure kwa chanjo ya Tatu moja ambapo wafugaji watatoa shilingi 500 tu kwa dozi ya  chanjo ya ng'ombe na shilingi 300 kwa dozi ya mbuzi na kondoo.

Naye Ndg. Haruna Haji  ambaye ni Mkuu wa Divisheni ya Biashara, viwanda na Uwekezaji kwa niaba ya Bi. Happiness R. Laizer Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, amesema kuwa kama Halmashauri tunakiri kupokea hivyo vifaa na wataalam wamejipanga  kuhakikisha zoezi hili litafanyika kwa ufanisi mkubwa. Hivyo ninawaomba Wananchi wapokee chanjo hizi ili kazi iende sawa sawa.

Kwa upande wake Bi. Marselina Shangali (wa kwanza kulia) ambaye ni mmoja wa wafugaji wa kuku Wilayani Monduli ameeleza kuwa yeye awali alikuwa anafuga kuku pasipo kuzingatia chanjo na hivyo ufugaji wake haukuwa na tija kwani kuku wengi walikufa. Hivyo kupitia chanjo hizi ninatarajia kufuga kwa tija na ufugaji wangu utakuwa wa viwango.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI ZA UJENZI ZAPEWA MAFUNZO - MONDULI

    July 16, 2025
  • DC GLORIANA AZINDUA CHANJO YA TATU MOJA- MONDULI

    July 16, 2025
  • MHE. GLORIANA KIMATH AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    July 08, 2025
  • MONDULI YANG'ARA MATOKEO YA MITIHANI YA TAIFA 2024 MA 2025

    July 08, 2025
  • Angalia zote

Maktaba ya Video

UFUNDISHAJI WA SOMO LA HISABATI KWA VITENDO KWA DARASA LA NNE SHULE YA MSINGI MAZOEZI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • EDWARD MORINGE SOKOINE
  • TAARIFA YA UPANDAJI MITI
  • Historia ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
  • Mto Wa Mbu - Monduli ilivyonufaika na Tsh. Milion 400

Viunganishi linganifu

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya ajira ya Serikali
  • Ofisi ya Rais utumishi na utawala bora
  • salary slip portal
  • Tanzania Safari Channel

Waliotembelea Kiulimwengu

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Monduli District Council

    Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli

    Namba ya simu: +255 - 27- 2538006

    simu ya mkononi:

    Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz

Mawsilano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Malalamiko
    • ramani ya eneo
    • Huduma zetu

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli