• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Monduli District Council
Monduli District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Malengo
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Eneo la Utawala
      • Tarafa
      • Kata
      • Vijiji
    • Idara
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Idara ya Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwezekaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Onana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelezwa
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria ndogo
    • Mipango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA USHAURI WILAYA (DCC) YAPONGEZA USIMAMIZI NA UKUSANYAJI MAPATO MONDULI

Posted on: February 13th, 2025

Ndg. Anael Mbise Afisa Tawala Wilaya ya Monduli kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya DCC Wilayani humo Mhe. Festo Shem Kiswaga leo Feb. 2025 katika Ukumbi wa Halmashauri hiyo, ameongoza kikao cha Kamati hiyo chenye lengo la kujadili na kupitisha mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri hiyo kwa Mwaka wa fedha 2025/2026.

Akizungumza katika kikao hicho Ndg. Anael Mbise amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kwa ufuatiliaji, usimamizi na kukusanya mzuri wa mapato yeye pamoja na Watendaji wake wote na kupelekea kuongezea kwa makusanyo Wilayani humo kwa ongezeko la asilimia 3.9 kutoka asilimia 3.0

Aidha, Ndg. Anael Mbise amewataka Maafisa Watendaji wote wa Kata na Vijiji kumsaidia Mkurugenzi kuhakikisha wanasimamia vizuri ulipaji wa ushuru wa Mifugo katika maeneo yao kwa kuwa kama jitihada zitaongezeka Halmashauri inaweza kuvuka kiwango cha bilioni 3.9 hadi kukamilisha bilioni 4 na hili litawezekana zaidi kwa kuziba mianya ya rushwa kwa kutoa risiti kwa kila malipo yanayofanyika.

Akiwasilisha mapendekezo ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2026 Ndg. Lucas Daud (DPLO) katika Halmashauri hiyo, amewapitisha wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Wilaya hiyo (DCC) kwenye Bajeti ya 2023/2024 kwa kueleza mafanikio, changamoto na ufumbuzi wake, sambamba na kueleza mapitio ya nusu mwaka ya Bajeti ya 2024/2025 yenye jumla ya Tsh. Bilioni 46.5

Ndg. Lucas amebainisha kuwa kwa Mwaka wa fedha 2025/2026 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli imekusudia kukusanya na kutumia jumla ya shilingi bilioni 48.1 ambayo ina ongezeko la asilimia 3.4 ukilinganisha na bilioni 46.5 kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Naye Bi. Happiness R. Laizer Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli ametoa shukrani kwa Menejimenti, Watendaji wa Kata na Vijiji na wote wanaohusika katika ukusanyaji wa mapato kwa ushirikiano mzuri uliopelekea ufanisi katika  zoezi la ukusanyaji mapato ambapo kufikia Disemba 2024 Halmashauri ilikuwa imefikia asilimia 75 ya malengo ya makusanyo.

Aidha, Bi. Happiness ameshukuru Serikali ya awamu ya 6 ya uongozi makini wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia asilimia 100 ya fedha za Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri yetu ya Monduli.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DC MONDULI AWAPONGEZA MADAKATRI BINGWA WA MAMA SAMIA

    May 17, 2025
  • ELIMU YA LISHE, AFYA NA MAZINGIRA PAMOJA NA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE IENDELEE KUTOLEWA- MONDULI.

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA 3

    May 14, 2025
  • MAMALISHE 30 WAPATIWA MAJIKO YA NISHATI SAFI -MONDULI

    May 14, 2025
  • Angalia zote

Maktaba ya Video

UFUNDISHAJI WA SOMO LA HISABATI KWA VITENDO KWA DARASA LA NNE SHULE YA MSINGI MAZOEZI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • EDWARD MORINGE SOKOINE
  • TAARIFA YA UPANDAJI MITI
  • Historia ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
  • Mto Wa Mbu - Monduli ilivyonufaika na Tsh. Milion 400

Viunganishi linganifu

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya ajira ya Serikali
  • Ofisi ya Rais utumishi na utawala bora
  • salary slip portal
  • Tanzania Safari Channel

Waliotembelea Kiulimwengu

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Monduli District Council

    Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli

    Namba ya simu: +255 - 27- 2538006

    simu ya mkononi:

    Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz

Mawsilano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Malalamiko
    • ramani ya eneo
    • Huduma zetu

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli