• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Monduli District Council
Monduli District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Malengo
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Eneo la Utawala
      • Tarafa
      • Kata
      • Vijiji
    • Idara
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Ardhi na Mali Asili
      • Idara ya Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwezekaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Ujenzi, Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
      • Onana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelezwa
  • Machapisho
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria ndogo
    • Mipango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MONDULI YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI

Posted on: June 14th, 2025

Ninawapongeza sana kwa hatua hii kubwa mliyoifikia ya kupunguza vifo vya akina Mama na watoto wachanga vinavyotokana na uzazi kutoka vifo vitatu(3) hadi kimoja(1) pamoja na kuongeza idadi ya Wanawake wanaojifungulia katika hospitali zetu kutoka 4,476 hadi 5,900 kwa mwaka 2023/2024.

Hayo yamesemwa leo Juni 14, 2025 na Bi. Pamela Ijumba kwa niaba ya Bi. Happiness R.  Laizer Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli,  alipokuwa akizungumza na Wauguzi wa vituo vya afya na wa hospitali ya Wilaya hiyo katika maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani ambayo Ki Wilaya yamefanyika katika viwanja vya kituo cha afya Mto wa Mbu Wilayani humo.

Bi. Pamela amewaeleza Wauguzi hao kuwa, " Ninyi ni injini katika Idara ya Afya kutokana na umuhimu wenu kwa kusaidia kuokoa maisha ya watu Duniani hivyo tunatarajia kuwa mntaendelea kutoa huduma kwa wagonjwa kwa kuzingatia Sheria, miongozo, na taratibu kama alivyofanya mwasisi wenu Bi. Florence Nightingale." amesema Bi. Pamela

Akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi kwa niaba ya Mwenyekiti wa Wauguzi hao

Bi. Epifania Mratibu wa afya ya Uzazi Wilaya, ametaja mafanikio makubwa yaliyofikiwa kwa mwaka 2025 kuwa ni pamoja :- kufanya kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na Uzazi kutoka vifo vitatu hadi kimoja kwa mwaka 202/2024, kuongeza idadi ya wamama wanaojifungulia hospitali kutoka 4,476 hadi 5,900 kwa mwaka 2023/2024, kukusanya damu salama, kufanya uchunguzi wa saratani ya mlango wa Uzazi na matiti, uchunguzi wa homa ya ini na kutoa chanjo yake, kutoa huduma ya dawa za ganzi na usingizi, kupima shinikizo la damu, kutoa elimu ya Malezi na Makuzi pamoja na kuhudumia wagonjwa wa ndani na wa nje.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. George Kasibante amewataka Wauguzi hao kutoa huduma bora kwa wagonjwa, kujitoa, na kwa wale ambao bado hawawajibiki vizuri wabadilike haraka sana kwakuwa Mazingira ya kazi yameboreshwa, dawa zipo, na miundombinu imeboreka katika kila vituo vya afya

Naye Bi.  Rose Yongolo Mwenyekiti wa Wauguzi hao amewashauri Wauguzi wenzake kufanya kazi kwa kufuata maadili na mienendo ya mwasisi wao Bi. Florence Nightingale huku akieleza kuwa mishumaa waliyoiwasha wakati wa kula kiapo cha uadilifu iwakunbushe namna ambavyo Bi. Florence alitumia Nuru hiyo kwenda kila mahali kutoa huduma kwenye vita ya pili ya Dunia - Cremean war vivyo hivyo na wao watoe huduma kwa wagonjwa.

Bi. Pamela Ijumba amehitimisha kwa kuwataka Wauguzi hao walio tayari kujifunza suala la utoaji wa ganzi tiba na usingizi kufanya hivyo kwani Bajeti ipo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rc KIHONGOSI APOKELEWA KWA SHANGWE MKOANI ARUSHA.

    June 30, 2025
  • Rc KIHONGOZI APOKELEWA KWA SHANGWE MKOANI ARUSHA.

    June 30, 2025
  • MHE. FREDRICK LOWASSA AZINDUA MRADI WA NYUMBA YA WAHUDUMU ARKARIA.

    June 26, 2025
  • MONDULI YATOA ELIMU YA BIASHARA KIDIJITALI

    June 20, 2025
  • Angalia zote

Maktaba ya Video

UFUNDISHAJI WA SOMO LA HISABATI KWA VITENDO KWA DARASA LA NNE SHULE YA MSINGI MAZOEZI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • EDWARD MORINGE SOKOINE
  • TAARIFA YA UPANDAJI MITI
  • Historia ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
  • Mto Wa Mbu - Monduli ilivyonufaika na Tsh. Milion 400

Viunganishi linganifu

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya ajira ya Serikali
  • Ofisi ya Rais utumishi na utawala bora
  • salary slip portal
  • Tanzania Safari Channel

Waliotembelea Kiulimwengu

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Monduli District Council

    Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli

    Namba ya simu: +255 - 27- 2538006

    simu ya mkononi:

    Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz

Mawsilano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Malalamiko
    • ramani ya eneo
    • Huduma zetu

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli