Ninawataka muendelee kuwa msaada katika Jamii kwa kusaidia kutatua migogoro ikiwemo migogoro ya ardhi, ndoa, familia yaani ndugu kwa ndugu na mirathi kwa kuwa utatuzi wa migogoro hii unahitaji zaidi busara za wazee.

Hayo yamesemwa leo Septemba 25, 2025 na Ndg. Muhsin Kassim Katibu Tawala kwa niaba ya Mhe. Gloriana J. Kimath Mkuu wa Wilaya ya Monduli katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika Mjini humo katika Ukumbi wa CDTI.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za wazee katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Ndg. Constantino Rahhi Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya, amesema kuwa Halmashauri hiyo ina jumla ya Wazee 13,160 kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ambayo inabainisha jumla ya Wazee 4,306 wasiojiweza na ambao wamepewa vitambulisho vya matibabu bure.
Aidha, kwa mwaka 2025 Halmashauri kupitia Kitengo cha Ustawi wa Jamii imeendelea kutekeleza Afua za Wazee kwa njia ya matangazo katika hospitali, vituo vya Afya na zahanati kwa kuwapa wazee kipaumbele ' Mzee kwanza: mpishe Mzee apate huduma. " , kuhakikisha mwakilishi mmoja anahudhuria Maadhimisho haya Kitaifa Mkoani Ruvuma. kupinga ukatili, kuwezesha vikao vya robo vya baraza wazee la Wilaya, kuwezesha wazee 420 kupata BIMA za Afya za ICHF pamoja na kutoa matibabu bure kwa wazee.
Naye Ndg. Hamisi Ramadhani Mwenyekiti wa Baraza la Wazee ameiomba Serikali kwa ngazi ya halmashauri kuwapatia mikopo kupitia vikundi vya ujasiriamali, kwakuwa wazee wanachangamoto ya hali duni ya maisha kwa kukosa mitaji; huku akiomba wazee kushirikishwa katika vikao vya maamuzi.

Akijibu kipengele cha ushiriki wa wazee katika vikao, Bi. Pamela Ijumba, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli amewaeleza Wazee hao kuwa wanayofursa ya kushiriki katika mabaraza ya wazi ya Halmashauri kwakuwa vikao vingine vipo kwa mujibu wa Sheria huku akiwataka kuomba nafasi katika ngazi za vijiji na Kata (kwa vituo vyote vya Afya) ili wapate fursa za kushauri masuala ya maendeleo na Afya.
Kwa upande wake Dkt. George Kasibante Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo amewaeleza Wazee hao kuwa kwa sasa huduma ambazo awali walizifuata Mount Meru hospitali kama vile huduma ya mazoezi, vipimo vya meno, kifua, na uchungizi wa damu zinaoatikana katika hospitali ya Wilaya pamoja na kuwepo kwa Daktari Maalum wa kuhudumia wazee., huku akibainisha kuwa vipimo hivyo pia vinapatikana katika vituo vya Afya vya NAFCO, Makuyuni na Mto wa Mbu
Kaulimbiu: " Wazee tushiriki Uchaguzi kwa Ustawi wa Jamii



Monduli District Council
Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli
Namba ya simu: +255 - 27- 2538006
simu ya mkononi:
Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli