Leo tarehe 23 Oktoba 2025, Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Mhe. Gloriana Kimath ameongoza kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za lishe kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 (Julai – Septemba) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Katika kikao hicho Mhe. Gloriana amewataka watendaji wa kata kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao na kuwa SMART kwakuzingatia uadilifu kazini ili kuongeza ufanisi katika kufanya kazi zao.
Afisa Lishe wa Wilaya ya Monduli, Bw. Michael Muhombo akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2025 alieleza mafanikio yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kuvuka kiwango cha asilimia 100 walichojiwekea cha matumizi kwa asilimia 183, pamoja na kuwajengea uwezo Watumishi katika masuala ya Lishe sambamba na kueleza changamoto mbalimbali zilizojitokeza, pamoja na mikakati ya kuboresha hali ya lishe kwa wananchi.
Aidha, Bi. Namnyaki Laitatei Mkuu wa Divisheni ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu amewataka watendaji wa kata kuwasilisha taarifa iwapo kama kuna wananchi waliopo kwenye maeneo yao ambao wanamiliki mashine za kuongeza virutubisho kwenye chakula, ili kuwezesha utayarishaji wa vyakula vyenye virutubisho kwa ajili ya wanafunzi mashuleni.
Monduli District Council
Sanduku la Posta: P.O BOX 1 Monduli
Namba ya simu: +255 - 27- 2538006
simu ya mkononi:
Barua Pepe: ded@mondulidc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Monduli